Na Mwandishi wetu, timesmajira
Waziri wa Afya Ummy Mwalimu leo Octoba 4,2023 amepokea magari 10 ya kubebea wagonjwa yenye thamani ya Shilingi Bil. 1.1 kutoka Serikali ya India.
Waziri Ummy ameishukuru Serikali ya India kupitia kwa Balozi wa India nchini Mhe. Binaya Pradhan kwa msaada huo ambao unaendelea kuonesha ushirikiano baina ya nchi hizo mbili.

“Serikali ya India imekua na ushirikiano Mkubwa na Serikali ya Tanzania ikiwemo katika Sekta ya Afya, hivyo nitumie fursa hii kuwashuku sana kwa msaada wa magari haya ambayo hata kwenda kusaidia kurahisisha huduma kwa Watanzania”.Amesema Waziri Ummy

More Stories
Wapambe waanza rafu za uchaguzi Morogoro Mjini
Daraja la J.P.Magufuli kuzinduliwa Juni 19,2025
Yas yazidi kuboresha huduma sekta ya Utalii