Na Mwandishi wetu, TimesMajira Online
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan leo Agosti 15,2024 amewasili Harare Nchini Zimbabwe ambako atashiriki Mkutano wa 44 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC).
Katika Mkutano huo utakao fanyika Agosti 17, Rais Samia atapokea kiti cha Uenyekiti wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya SADC kutoka kwa Rais wa Zambia, Hakainde Hichilema.
More Stories
Mwabukusi:Kufanyakazi kwa kushirikiana na serikali siyo kulamba asali
Waislamu wamuombea dua Rais Samia,wasisitiza umoja
Samia: Serikali imejifunza somo kuporomoka ghorofa