Na Mwandishi Wetu,Timesmajiraonline
RAIS Samia Suluhu Hassan amekabidhi cheti cha pongezi kwa ushiriki wa Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) kwenye tamasha la Kizimkazi Festival 2024, wakati wa Hafla ya chakula cha usiku iliyofanyika Ikulu ndogo Kizimkazi Zanzibar.
Cheti hicho cha pongezi kimepokelewa kwa niaba ya Kamishna wa Uhifadhi wa TANAPA, Nassoro Juma Kuji, na Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi, Jully Bede Lyimo – Mkuu wa kitengo cha Maendeleo ya Biashara pamoja na Afisa Uhifadhi Mwandamizi Amina R. Salum ambaye ni Afisa Utalii Hifadhi ya Taifa Ruaha.
TANAPA, kwa dhati na unyenyekevu mkubwa tumepokea na kuthamini heshima hii kubwa kutoka kwa Dkt Samia Suluhu Hassan.
More Stories
Airtel Afrika yateua Publics Groupe Africa kuwa mbia wake katika masoko 12 Barani Afrika
Watu wanne mbaroni kwa tuhuma za wizi wa vifaa vya mradi Miji 28
TRA yabaini ukwepaji kodi mkubwa viwandani