Na Mwandishi wetu, TimesMajira Online
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, ameiagiza serikali yake kuhakikisha Serikali ya Mkoa na Kitengo cha Maafa cha Ofisi ya Waziri Mkuu kuweka makazi ya muda ya watu ambao makazi yao yamesombwa na maji kwa lengo la kuwastiri wananchi hao wilayani Hanang, mkoani Manyara, haswa katika vijiji vya Katesh, Jorodom, Ganana, Dumbeta, Gendabi, Sarijandu, Arukushay na Sebasi.
Kwa taarifa za awali nyumba na mifugo imeathirika sana huku idadi za kaya zilizoathirika ni 1,150, idadi ya watu walioathirika hadi sasa ni 5,600 na pia ikikadiriwa takriban ekari 750 za mashamba zimeharibika.
More Stories
Lwahima,waanza kupata maji
Naibu Kadhi Mkuu ampongeza Shiraz kwa kujenga Msikiti Dar
Green Acres kuonyesha maajabu mitihani ya la 7, kidato cha nne