Na Mwandishi wetu, TimesMajira Online
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, ameiagiza serikali yake kuhakikisha Serikali ya Mkoa na Kitengo cha Maafa cha Ofisi ya Waziri Mkuu kuweka makazi ya muda ya watu ambao makazi yao yamesombwa na maji kwa lengo la kuwastiri wananchi hao wilayani Hanang, mkoani Manyara, haswa katika vijiji vya Katesh, Jorodom, Ganana, Dumbeta, Gendabi, Sarijandu, Arukushay na Sebasi.
Kwa taarifa za awali nyumba na mifugo imeathirika sana huku idadi za kaya zilizoathirika ni 1,150, idadi ya watu walioathirika hadi sasa ni 5,600 na pia ikikadiriwa takriban ekari 750 za mashamba zimeharibika.
![](https://timesmajira.co.tz/wp-content/uploads/2023/12/IMG-20231204-WA05141.jpg)
![](https://timesmajira.co.tz/wp-content/uploads/2023/12/IMG-20231204-WA0517.jpg)
![](https://timesmajira.co.tz/wp-content/uploads/2023/12/IMG-20231204-WA0516.jpg)
![](https://timesmajira.co.tz/wp-content/uploads/2023/12/images-9.jpeg)
More Stories
Kituo cha mfano Katente chaongeza makusanyo MBOGWE
Elimu ya fedha yawafikia wananchi wa Makanya wilayani Same
Wasira:Uchaguzi Mkuu utafanyika wanaCCM,Wananchi jiandaeni