Na Mwandishi Wetu, TimesMajira Online
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Alhaj Othman Masoud Othman, leo Julai 31, 2022 amejumuika na Viongozi na Waumini mbalimbali wa Kiislamu, wakiongozwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dkt. Husein Ali Mwinyi, katika Kongamano maalum la Kuadhimisha Mwaka Mpya wa Kiislamu wa 1444 Hijria.

Kongamano hilo ambalo limeandaliwa na Ofisi ya Mufti Mkuu Zanzibar, na kubeba Mada ya “Mafunzo ya Hijra kwa Waislamu”, linafanyika katika Masjid Jamiu Zinjibar, Msikiti uliopo Mazizini, Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja.
More Stories
Chalamila:Dar ni salama,aelezea mafanikio na mipango ya maendeleo ya Mkoa
Ulaji vyakula vya aina moja,umri vyatajwa ongozeko la matatizo ya macho Mbeya
Kenya,Uganda zaanzisha mradi wa uendelezaji rasilimali za maji Angololo