Na Mwandishi wetu, TimesMajira Online
Kwa mara ya kwanza nchini, tumezindua rasmi NMB Jiwekee, yenye lengo la kuhifadhi pesa kidijitali kwa ajili ya maisha ya baadae.
Kupitia NMB Jiwekee, mteja ataweza:
➡️ Kuweka kati ya asilimia 1-100 ya kipato kinachoingia kwenye akaunti yake na anaweza kubadilisha muda wowote
➡️ Kuhifadhi hela kwenye NMB Jiwekee kuanzia miaka 5 na kuendelea
➡️ Kuvuna riba shindani na ataipata kila baada ya miezi mitatu
➡️ Kusitisha uchangiaji kwa muda kutokana na mahitaji, bila ya kutoa pesa zake kwenye NMB Jiwekee, na ataweza kuendeleza uchangiaji wakati wowote kupitia NMB Mkononi
➡️ Hakuna kiingilio wala makato
➡️ Kuweka amana katika NMB Jiwekee kupitia mitandao ya simu, benki zingine na mifumo yetu yote.
➡️ Kuangalia salio na taarifa za michango yako kupitia NMB Mkononi.

Uzinduzi huu umeongozwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu – Mhe. Deo Ndejembi na Afisa wetu Mkuu wetu wa Wateja Binafsi na Biashara- Filbert Mponzi.
Pia, mahojiano yaliongozwa na Millard Ayo huku mada za utunzaji pesa zikitolewa na Lamata Leah pamoja na Masoud Kipanya.


More Stories
Vitongoji Musoma vijijini vyaendelea kuunganishiwa umeme
Mpango mahsusi wa Taifa kuhusu Nishati wajadiliwa
Mwenyekiti CCM, Mbunge Rorya wavuruga mafunzo ya makatibu