Na Mwandishi Wetu, TimesMajira Online
MWANAMUZIKI mkongwe katika muziki wa dansi na mbobezi kwenye kupiga gitaa la solo kwenye bendi ya Msondo Ngoma, Said Mabera amefariki dunia usiku wa kuamkia leo.
Akizungumza na TimesMajira Online kwa njia ya simu, meneja wa bendi ya Msondo Ngoma Said Kibiriti, amethibitisha taarifa hiyo na kusema kuwa Mabera aliaga dunia majira ya saa 6 kasoro usiku wa kuamkia leo.
Hata hivyo, kwa mujibu wa Kibiriti, marehemu Mabera alisimama kufanya shughuli zake za muziki takribani miezi miwili iliyopita kutokana na Afya yake kutrokuwa nzuri mpaka umauti unamfika, hivyo anatarajiwa kuzikwa leo saa 10 jioni nyumbani kwake Mbezi mwisho.
%%%%%%%%%%
More Stories
Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM wakiburudika kusubiri Uzinduzi Ilani ya CCM 2025-2030
Mwanamitindo Millen Magese apewa kibali kuandaa Miss Universe Tanzania 2025
Pacha Milionea waja na truck mpya “Nyumbani”