Na Mwandishi wetu,Dar es Salaam
Hospitali ya Taifa Muhimbili imefanya upasuaji mkubwa wa kuondoa bandama lenye shida kwa mgonjwa kwa njia ya matundu madogo (laparoscopic splenectomy).
Upasuaji huu ni wa kwanza kufanyika hapa nchini ambao umefanywa na madaktari wa upasuaji wa MNH kutokana na ubobezi walionao.
Dkt. Kitembo Salum Kibwana mbobezi wa upasuaji mfumo wa chakula na Ini ndiye aliyeongoza jopo la madaktari, wauguzi na watalaamu wa ganzi na usingizi kufanya Upasuaji huo.

Bandama (wengu) ni kiungo cha mwili chenye nafasi katika mzunguko wa damu. Lipo ndani ya fumbatio ya mwili karibu na mfuko wa chakula ambapo kazi yake kubwa ni kuongeza seli nyeupe za damu na kuondoa seli nyekundu za damu zilizozeeka.
Kwa watoto ina jukumu la kutengeneza seli nyekundu za damu. Watu wazima kwa kawaida wanaweza kuishi bila ya bandama.
Hospitali ya Taifa Muhimbili inaendelea kuboresha huduma zake mbalimbali ikiwemo upasuaji mkubwa, uchunguzi na mifumo ya utoaji huduma kwa ujumla wake.
More Stories
Papa Francis afariki Jumatatu ya Pasaka akiwa na miaka 88
Kanisa la Shincheonji la Yesu nchini Ufaransa lakanusha ripoti ya Le Parisie
Vyombo vya ulinzi na usalama Mbeya,Benki kuu kushirikiana kutatua changamoto za utapeli mtandaoni