June 26, 2024

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Mfahamu Msemaji mpya wa Serikali

Na Mwandishi wetu, TimesMajira Online

Thobias Makoba, ameteuliwa kuwa Mkurugenzi wa Idara ya Habari – Maelezo na Msemaji Mkuu wa Serikali.

Makoba anachukua nafasi ya Mobhare Matinyi ambaye amepangiwa majukumu mengine.

Kabla ya Uteuzi huu Makoba alikuwa Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano katika Ofisi ya Msajili wa Hazina.

Kabla ya kujiunga na Ofisi ya Msajili wa Hazina, Makoba alikuwa Afisa Mambo ya Nje Mwandamizi katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Pamoja na kushiriki katika majukwaa mbalimbali ya Kimataifa ikiwemo UN, African Union, SADC, EAC, World Economic Forum na mengineyo, kwa vipindi mbalimbali aliwahi kuwa Katibu wa Mawaziri wawili wa Mambo ya Nje Bernard Membe na baadae Balozi Dokta Augustine Mahiga kabla ya Kwenda kuwa Kaimu Mkurugenzi Msaidizi katika Ofisi ya Mambo ya Nje Zanzibar.

Makoba ana Masters Degree in Security and Strategic Studies kutoka National Defence College – Tanzania, Post-Graduate Diploma in Economic Diplomacy kutoka Chuo Cha Diplomasia Kurasini na Degree ya kwanza ya Political Science and Sociology with majors in International Relations.