October 6, 2024

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan (kushoto), akimsikiliza Meneja Msaidizi Uhusiano na Itifaki Benki Kuu ya Tanzania BoT, Vicky Msina (katikati) huku Naibu Gavana wa BoT, Dkt. Bernard Kibesse (kulia) akishuhudia wakati Kiongozi huyo alipotembelea banda la Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kwenye viwanja vya Nyakabindi nje kidogo nya mji wa Bariadi mkoani Simiyu ambako maonesho ya Nane Nane Kitaifa mwaka huu wa 2020 yanafanyika. Makamu wa Rais amefungua rasmi maonesho hayo leo.

Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan atembelea banda la BoT Nane Nane

Na Khalfan Said, Nyakabimdi

MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ametembelea banda la Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kwenye Viwanja vya Nyakabindi nje kidogo ya mji wa Bariadi Mkoani Simiyu.

Makamu wa Rais ametembelea banda hilo leo wakati wa ufunguzi wa maonesho ya mwaka huu ya Nane Nane yanayofanyika Kitaifa kwenye viwanja hivyo.

Makamu wa Rais amepokewa na Naibu Gavana wa Benki Kuu, Dkt. Bernard Kibesse na Meneja Uhusiano na Itifaki BoT, Zalia Mbeo ambapo ametembelea idara mbalimbali za Benki hiyo na kuelezwa jinsi zinavyowahudumia wananchi wanaofika kwenye banda hilo.

Meneja Uhusiano na Itifaki BoT, Zalia Mbeo (kushoto) akimuongoza Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan kutembelea banda hilo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan (kushoto) akipokea mfuko wenye machapisho mbalimbali yanayoelezea shughuli za BoT kutoka kwa Naibu Gavana wa Benki Kuu, Dkt. Bernard Kibesse wakati alipotembelea banda hilo leo.
Makamu wa Rais akiondoka wkenye banda la BoT baada ya kulitembelea.

Maonesho ya mwaka huu ambayo yamebeba kauli mbiu isemayo; “Kwa Maendeleo ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi Chagua Viongozi Bora 2020.”

Lengo hasa la maonesho hayo yanayofanyika kitaifa kwa mara ya tatu mfululizo kwenye viwanja hivyo ni kutoa fursa kwa wakulima, wafugaji, wavuvi na wanaushirika kuona na kujifunza matumizi ya teknolojia bora za kilimo, ufugaji na uvuvi kwa ajili ya kuongeza tija na uhakika wa chakula na kukidhi mahitaji ya viwanda na masoko.