Na Mwandishi wetu TimesMajira Updates
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyabiashara wa Madini Tanzania (TAMIDA) Osman AbdulSattar Tharia ametembelea banda la Tanzania kwenye maonesho ya Expo 2020 Dubai ambapo amepolekewa na Mkurugenzi wa Banda la Tanzania Getrude Ng’weshemi kutoka TanTrade pamoja na wawakilishi wa Sekta mbalimbali zinazoshiriki kwenye maonesho haya.
Osman amefurahi kuona Tanzania imeshiriki miongoni mwa nchi 192 ikiwa na banda lake linalovutia kwa kuonesha jinsi sekta kadhaa zimeonesha rasilimali mbalimbali zilizopo nchini.

Amesema,” Kwa upande wa Sekta ya Madini, mmeitumia vizuri fursa hii kuonesha ‘Tanzanite’ kwani ni moja ya madini adimu na yenye thamani ulimwenguni. Naunga mkono ushiriki huu na ujio wangu hapa leo utaenda kuongeza msukumo nyumbani wa kuendelea kuhamashisha ushiriki wa uhakika na wenye tija hasa ushiriki katika Wiki ya Madini iliyopangwa kufanyika tarehe 22 Desemba, 2021 mpaka tarehe 4 Januari, 2022 ambapo wadau wote wa Madini wa fursa ya kuja Dubai kushiriki kwenye programu zilizoandaliwa. Nafasi hii tuliyopata tuitumie kikamilifu kuitangaza nchi yetu na rasilimali zitakazofungua fursa mbalimbali ulimwenguni”.
More Stories
Kampeni ya kisheria ya Mama Samia kuondoa migogoro na ukatili
Dc.Shaka akagua Miradi ya Maendeleo na kusikiliza Wananchi Kiduhi
Zaidi ya bilioni 40 kutatua kero ya maji Kasulu