Na Mwandishi wetu, TimesMajira Online
KATIBU Mkuu wa Wizara ya Madini Nchini, Kheri Mahimbali, amesema Tanzania kwa sasa imeweka mazingira mazuri kwa wawekezaji kuja kuwekeza kwenye sekta ya madini kwa namna itakayofaidisha pande zote.
Mahimbali ameyasema hayo wiki hii wakati wa mkutano wa wadau wa sekta ya madini uliondaliwa na taasisi ya Chatham House na uliofanyika jijini London.

Katika mkutano huo, Katibu Mkuu Mahimbali amezungumzia umuhimu wa kuongezeka kwa uwekezaji kwenye madini ya kimkakati ambayo yako kwa wingi ambao uwekezaji wake umekuwa mdogo ukilinganisha na mahitaji yaliyopo hasa barani Afrika.
More Stories
Ujenzi Maabara za masomo ya sayansi waendelea Musoma Vijijini
TBS:Majibu ya sampuli kutoka TBS yanaamika kokote duniani
Waziri Mkuu mgeni rasmi maadhimisho ya siku ya misitu Duniani