Na Mwandishi wetu, TimesMajira Online
KATIBU Mkuu wa Wizara ya Madini Nchini, Kheri Mahimbali, amesema Tanzania kwa sasa imeweka mazingira mazuri kwa wawekezaji kuja kuwekeza kwenye sekta ya madini kwa namna itakayofaidisha pande zote.
Mahimbali ameyasema hayo wiki hii wakati wa mkutano wa wadau wa sekta ya madini uliondaliwa na taasisi ya Chatham House na uliofanyika jijini London.
Katika mkutano huo, Katibu Mkuu Mahimbali amezungumzia umuhimu wa kuongezeka kwa uwekezaji kwenye madini ya kimkakati ambayo yako kwa wingi ambao uwekezaji wake umekuwa mdogo ukilinganisha na mahitaji yaliyopo hasa barani Afrika.
More Stories
Wananchi,Viongozi Musoma vijijini waishukuru serikali ujenzi miradi ya maji
Waomba fomu zenye maandishi ya nukta nundu
Mnyeti agawa madume bora ya Ng’ombe 40 kwa wafugaji Serengeti na Bunda