Na Mwandishi Wetu
WATU milioni 50 Ulimwenguni (sawa na asilimia 0.7 ya watu wote duniani) wamelewa pombe muda huu wakati unaposoma taarifa hii.
Kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani (WHO), pamoja na kwamba Bara Ulaya ndio linaongoza kwa unywaji pombe zaidi, Bara la Afrika ndilo lenye mzigo mkubwa zaidi wa madhara yanayotokana na unywaji pombe kama vile vifo, majeraha na athari nyingine zizokanazo na ajali za barabarani.
Hata hivyo ripoti hiyo inayotolewa WHO kila mwaka ijulikanayo kama Ripoti ya Hali ya Kiafya na Unywaji Pombe Duniani (Global Status Report on Alcohol and Health) inaeleza kwamba asilimia 45 ya watu Ulimwenguni hawajawahi kunywa pombe, ambapo asilimia 35 ni wanaume na wanawame ni asilimia 55.
Kwa maana hiyo ni kwamba nusu ya wanaume na theluthi mbili ya wanawake wote duniani wameweza kujizuia na unywaji pombe kwa mwaka (miezi 12). Tafakari, wewe na mimi upo kwenye kundi lipi kati ya wanaokunywa pombe na wasiokunywa?
More Stories
Coca-Cola Kwanza kuwanufaisha mama lishe Stendi ya Msamvu Marogoro
Sheikh Ponda akabidhiwa kadi ya heshima ya Maalim Seif
Sheikh Ponda kutua rasmi Act Wazalendo