Na Mwandishi wetu, TimesMajira Online
Serikali imesema kukamilika kwa kituo cha kupoza umeme cha Nyakanazi mkoani Kagera imepelekea kutenganisha matumizi ya umeme katika wilaya za Bukombe, Mbogwe, Biharamulo na Chato jambo ambalo limesaidia kila wilaya kujitegemea na pia kupunguza tatizo la kukatika kwa umeme katika Wilaya ya Biharamulo.
Naibu waziri wa Nishati, Judith Kapinga amesema hayo Bungeni Jijini Dodoma wakati akijibu maswali yaliyoelekezwa katika Wizara ya Nishati na Waheshimiwa Wabunge akiwemo Mbunge wa Jimbo la Biharamulo Eng. Ezra Chiwelesa.
![](https://timesmajira.co.tz/wp-content/uploads/2024/06/IMG-20240605-WA0874-1-1024x681.jpg)
Naibu Waziri Kapinga amesema kuwa TANESCO inaendelea na matengenezo ya kuimarisha miundombinu ya kusafirishia na kusambazia umeme katika Wilaya ya Biharamulo ili kuwe na umeme wa uhakika
More Stories
Rais Samia kufanya ziara ya kikazi Addis Ababa nchini Nigeria
Serikali ipo kwenye maandalizi ya TASAF III,ambao hawajainuka kiuchumi TASAF II kupewa kipaumbele
DC Kilindi ataka jitihada ziongezwe makusanyo mapato ya ndani