Na Mwandishi Wetu, TimesMajira Online, Shinyanga
MGOMBEA Ubunge katika Jimbo la Shinyanga Mjini kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Patrobas Katambi amedai alilazimika kuhama katika chama chake cha awali Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na kujiunga na CCM baada ya kuridhishwa na uchapaji kazi wa Rais Dkt. John Magufuli.
Katambi ametoa kauli hiyo kwenye mkutano wa kampeni za kunadi Sera na Ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020 – 2025 kwa wakazi wa Kata ya Ndembezi Manispaa ya Shinyanga ambao umefanyika katika Viwanja vya Ndembezi Migungani Manispaa ya Shinyanga.
Katambi amefafanua chanzo cha kudorora kwa uchumi wa wakazi wa Shinyanga ambapo amefafanua mikakati kadhaa ya kubadili hali hiyo na kwamba Jimbo la Shinyanga linahitaji watu makini ili wafanye kazi ngumu na hakuna njia ya mkato wala kutumia mapepo bali kwa kufanya kazi.
More Stories
Kamati ya kudumu ya Bunge ya utawala,katiba na sheria yaridhishwa ujenzi soko Kariakoo
TRA Tanga yakusanya bil.178.3 kwa miezi sita
Wataalam Sekta ya utalii watakiwa kufanya kazi kwa uadilifu,kujituma na kuwa wabunifu