Na Mwandishi wetu, TimesMajira Online
Wakati wa maonyesho ya biashara ya kimataifa yakifunguliwa na mgeni rasmi akiwa ni Rais wa Jamhuri ya Msumbiji Filipe Jacinto Nyusi aliyeambatana na mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan walitembelea mabanda mbalimbali kabla ya kufungua na kutoa zawadi kwa washindi mbali mbali.
Akizungumza wakati Marais hao wakitembelea banda lao Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya GF Trucks & Equipments Ltd , Imrani Karmali amesema baada ya ziara ya Rais nchini Korea
kushawishi wawekezaji kuwekeza nchini wao kama GF Automobile, wamezungumza na wakorea na wako tayari kuja kuweka kiwanda cha kuunganisha magari ya Hyundai nchini.
Amesema wakorea hao walitaka lazima kuwe na oda kubwa kwa kuanzia sasa ambapo wao kupitia kiwanda chao cha kunganishia magari cha GFA wapo tayari kufanya hivyo.
“Ombi letu kwako mama tunaomba Serikali kupitia wizara na tasisi zake kutuunga mkono katika hili na matunda ya ziara yako nchini korea kuonekana kwa Hyundani kutengenezwa nchini Tanzania”

More Stories
Kanisa la Shincheonji la Yesu nchini Ufaransa lakanusha ripoti ya Le Parisie
Vyombo vya ulinzi na usalama Mbeya,Benki kuu kushirikiana kutatua changamoto za utapeli mtandaoni
Polisi Mbeya kuimarisha ulinzi kuelekea sikukuu ya Pasaka