September 29, 2024

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Haki za wenye ualbino zitekelezwe

Na Bakari Lulela, TimesMajira Online

SERIKALI ya jamhuri ya muungano wa Tanzania itashirikiana na chama cha watu wenye ualbino kuhakikisha mapitio ya sera na haki za watu wenye ualbino zinatekelezwa kwa umakini mkubwa.

Akizungumza Mkoani pwani katika maadhimisho ya 19 mgeni rasmi mkuu wa mkoa huo Abubakari Kunenge aliyemuwakilisha waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu,kazi, vijana, ajira na wenye ulemavu amesema watu wenye ualbino ni jamii yetu hivyo Wana haki na wajibu wa kuishi katika Taifa hili.

“Serikali itaendelea kuyapa kipaumbele masuala yote yanayofanywa na watu wenye ualbino kwa kutambua kuwa wana haki ya msingi kuishi bila kubaguliwa na mtu yeyote,”amesema Kunenge

Aidha serikali iko makini katika kufuatilia mapitio ya sera mbalimbali na kukomesha vitendo hatarishi vinavyo hatarisha amani dhidi ya jamii ya watu wenye ualbino.

Hata hivyo watu hawa watashirikishwa katika mipango mbalimbali ya kimaendeleo kiuchumi iwe kuchugua ama kuchaguliwa katika chaguzi zilizo mbeleni mwetu.

Kwa upande wake mwenyekiti wa TAS Taifa Godson Mollel amesema Sheria za nchi zichukue nafasi kuwachukulia hatua walioshiriki utekaji wa tukio lililotokea Muleba kwa kumteka mtoto mwenye ualbino mwenye umri wa miaka 2 na nusu.

Ameendelea kusema wanamuomba rais dokta Samia Suluhu aweze kukutana na chama cha watu wenye ualbino kwa ajili ya kuzungumza nae masuala mbalimbali.

Mwenyekiti huyo amewataka watu wenye ualbino kuwa watulivu huku taratibu na hatua stahiki dhidi ya ulinzi wao ukichukuliwa na vyombo vya ulinzi na usalama na raia wema.

Mkuu wa mkoa wa pwani Abubakari Kunenge akikisisiza jambo katika maadhimisho ya siku 19 ya ualbino yaliyofanyika kibaha na kihudhuliwa na TAASISI mbalimbali na mamia ya watanzania
Mwenyekiti wa TAS Taifa Godson Mollel akisema jambo katika maadhimisho ya 19 siku ya ualbino