Na Agnes Alcardo, Timesmajira Online. Singida
Katibu mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Balozi Dkt Emmanuel Nchimbi akizungumza na Wananchi wa Kata ya Itaja, Jimbo la Singida Kaskazini, wakati akiwa njiani kuelekea Manyara ikiwa ni katika muendelezo wa ziara yake ya mikoa mitano.
Ziara ya Dkt Nchimbi inalenga kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo ambayo ipo ndani ya Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya 2020/2024 pamoja na kuzungumza na makundi mbalimbali ya Kijamii.
Kupitia ziara hiyo Balozi Dkt Emmanuel Nchimbi ameambatana na Katibu wa NEC Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa CCM Taifa, CPA. Amos Makalla pamoja na Katibu wa NEC, Mambo ya Siasa na uhusiano wa Kimataifa, Rabia Hamid.



More Stories
Kamati ya kudumu ya Bunge miundombinu,yaipa kongole Serikali ujenzi wa maabara ya Mawasiliano
Serikali kuzindua Sera ya Ardhi ya 1995 Toleo la 2023
Hospitali ya Rufaa Kanda ya Mbeya kuanzisha matibabu ya upasuaji moyo