Na Mwandishi wetu, TimesMajira Online
NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika mkutano 11 wa Kitaaluma wa Makatibu Mahsusi Tanzania.
Mkutano huo ambao unafanyika leo Mei 23,2024 katika uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.

Mkutano huo ulianz Mei 20, 2024, na unatarajiwa kuhitimishwa Mei 25, 2024 na unalenga kuimarisha utendaji kazi wa watumishi wa kada hiyo ikiwa ni pamoja na kusisitiza umuhimu wa kuzingatia maadili katika maeneo yao ya kazi.

Kaulimbiu ya mkutano huo ni “MAFANIKIO HUANZA NA UAMUZI BORA WA UTENDAJI, TUTUMIE MUDA VIZURI KWA KUFANYAKAZI NA KULETA TIJA”
More Stories
Waislamu Mwanza wapokea Ramadhani kwa maandamano ya kidini
Kamati ya kudumu ya Bunge ya utawala,katiba na sheria yaridhishwa ujenzi soko Kariakoo
TRA Tanga yakusanya bil.178.3 kwa miezi sita