Na Esther Macha, Timesmajira Online, Mbeya
Mhandisi Gwau amesema hayo leo wakati akizungumza na hili kwenye banda la Maonyesho ya sikukuu ya wakulima nane nane ambayo kitaifa inafanyika Jijini Mbeya.
Hata hivyo Mhandisi Gwau amesema kuwa kwa kuzingati changamoto za kitafiti katika uzalishaji Chuo hicho kina programu maalum ya kuangalia changamoto katika sekta ya kilimo na kuzitafutia majawabu lengo ni kuhakikisha inakuwa na wakulima kunufaika.
Eliwanzita Sospeter ni Mtaalam wa Teknolojia ya Chakula (MUST ) amesema kuwa wanatumia teknolojia za kisasa bunifu ya uzalishaji wa majokofu ambayo mkulima au mfanyashara ana uwezo wa kutunza mbogamboga na matunda kwa zaidi ya wiki moja pasipo kuharibika au kuathirika na wadudu.

Amesema kuwa ni Teknolojia ambayo ni rahisi kwa mkulima yeyote anasema kutumia na kuwa katika msimu wa maonyesho ya wakulima wamedhamiria kufanya ubunifu ili kuweza kuwasaidia wakulima.
Eliwanzita amesema kuwa katika msimu wa maonyesho haya Chuo cha Must wamejidhatiti kufanya ubunifu wa aina mbalimbali wenye kuleta matokeo mazuri katika Sekta ya kilimo.
Michael Raphael ni mkulima wa mboga mboga katika kata ya Igurusi amesema kuwa uwepo wa wataalamu kutoka Chuo cha Must umekuja Muda muafaka kwako kwani utaweza kuwasaidia katika uzalishaji pamoja na kilimo cha kisasa.
“Unajua ndugu mwandishi wakulima tuliowengi huko Vijijini tunajilimia tu bila kufuata taratibu za watalaam uwepo wa maonyesho haya naamini utatusaidia wakulima tulio wengi kubadilika baada ya kupata elimu”amesema.
More Stories
Benki ya NMB yatenga Bil. 100/-za nishati safi kwa wajasiriamali
Bussungu,Khatibu kupeperusha bendera ya ADA-TADEA uchaguzi Mkuu
Mwanasheria Mkuu wa Serikali Johari ameungana na Viongozi mbalimbali nchini kushiriki kuaga na kutoa heshima za mwisho kwa aliyekuwa Makamu wa Kwanza wa Rais Hayati Cleopa Msuya