Mwandishi wetu, Timesmajira online
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM ) kupitia Idala ya Itikadi na uenezi kimekabidhi Ngombe watano Kwa klabu ya Yanga na Ngombe mmoja wa klabu ya Simba ikiwa ni kutimiza ahadi ya Mkuu wa idala ya Itikadi na uenezi Paul Makonda aliyoitoa siku chache kabla ya mchezo wa watani wa jadi.
Akikabidhi Ngombe hao Kwa viongozi wa Klabu ya Yanga Jijini Dar es salaam Novemba 24 kwaniaba ya Mkuu wa idala ya Itikadi na uenezi Paul Makonda, katibu msaindizi Mkuu wa idala hiyo, Shaibu Akwilimbe amesema CCM kupitia Idala ya Itikadi na uenezi imekuja kutekekeleza ahadi yake ambayo iliitoa siku chache kabla ya mchezo wa watani wa jadi.

Amesema katika kuhamasisha michezo Mkuu wa Idala ya Itikadi na uenezi Paul Makonda aliwahidi Kila goli atatoa zawad ya Ngombe.
“Kwasababu ahadi ilikuwa Kila goli Ngombe mmoja nmekuja Kwa niaba yake kukabidhi Ngombe hawa watano Kwa viongozi wa yanga na mmoja Kwa klabu ya Simba”amesema
Akizungumza kwa niaba ya wazee wa Yanga, Mohamed Msumi alikishukuru Chama Cha Mapinduzi CCM kwa kutekekeleza ahadi yake na kueleza kuwa hiyo imedhiirisha Chama hicho kinafata misingi sahihi kwani michezo ni burudani.
“Chama Cha Mapinduzi CCM kimetimiza ahadi ya na wamefanya ilani ya Chama Cha Mapinduzi yenye sera ya michezo”amesema
Nakuongeza kuwa
“Goli hizi tato zimekuwa mpatanishi Kwa watani wa watani wetu wa jadi bila kuwapiga tano wasigejua wanamapugufu Gani”amesema Msumi

Aidha aliiomba klabu ya Simba kufuata mawazo na maoni ya wazee wao kama uongozi wa yanga unavyothamini wazee wake
More Stories
Rungwe yajenga soko kukuza uchumi kwa wananchi
Waislamu Mwanza wapokea Ramadhani kwa maandamano ya kidini
Kamati ya kudumu ya Bunge ya utawala,katiba na sheria yaridhishwa ujenzi soko Kariakoo