Na Mwandishi Wetu,TimesMajira Online. Ngara
SHILINGI bilioni 5.26, zimetolewa kupitia Wakala wa Barabara za Mjini na Vijijini (TARURA) kwa ajili ya ujenzi na matengenezo ya barabara katika Wilaya ya Ngara mkoani Kagera.
“Kati ya hizo, sh. bilioni 1.1 zimetengeneza barabara kwa kiwango cha lami kilomita 4.5 katika makao makuu ya wilaya hii.”
Hayo yamesemwa jana na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Kassim Majaliwa wakati akizungumza na wakazi wa Kata ya Rulenge, katika mikutano uliofanyika kwenye stendi ya Rulenge.
Amesema kiasi kingine cha sh. bilioni 4.16, zimetolewa kupitia TARURA kwa ajili ya ujenzi na matengenezo ya barabara ikiwemo Muhweza–Mukarehe, Keza–Nyanzovu, Mukalinzi–Mulonzi, Kibuba–Gwenzaza, Murugwanza-Runzenze (Airstrip), Chivu-Ntobeye–Nyakiziba, Buhororo– Mukididili, Ngara – Kumutana na Buhororo-Ruganzo (Airstrip).
More Stories
Kiongozi wa Mwenge awataka RUWASA kukamilisha mradi wa maji kwa wakati Kilindi
Balozi Nchimbi aongoza waombolezaji kumuaga Mzee Mongella
Ahukumiwa kunyongwa hadi kufa kwa kumuua mama yake mzazi