Na Mwandishi Wetu,TimesMajira Online. Ngara
SHILINGI bilioni 5.26, zimetolewa kupitia Wakala wa Barabara za Mjini na Vijijini (TARURA) kwa ajili ya ujenzi na matengenezo ya barabara katika Wilaya ya Ngara mkoani Kagera.
“Kati ya hizo, sh. bilioni 1.1 zimetengeneza barabara kwa kiwango cha lami kilomita 4.5 katika makao makuu ya wilaya hii.”
Hayo yamesemwa jana na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Kassim Majaliwa wakati akizungumza na wakazi wa Kata ya Rulenge, katika mikutano uliofanyika kwenye stendi ya Rulenge.
Amesema kiasi kingine cha sh. bilioni 4.16, zimetolewa kupitia TARURA kwa ajili ya ujenzi na matengenezo ya barabara ikiwemo Muhweza–Mukarehe, Keza–Nyanzovu, Mukalinzi–Mulonzi, Kibuba–Gwenzaza, Murugwanza-Runzenze (Airstrip), Chivu-Ntobeye–Nyakiziba, Buhororo– Mukididili, Ngara – Kumutana na Buhororo-Ruganzo (Airstrip).
More Stories
Rais Samia aridhishwa na utekelezaji miradi Tanga
Ziara ya Rais Samia yaanza kwa kishindo mkoani Tanga
Gambo: Rais Samia amefanya makubwa Jimbo Arusha Mjini