Na Mwandishi wetu, TimesMajira Online
Benki ya EQUITY imeendelea kurahisisha huduma zake katika nyanja zote kwa wadau wote wa biashara nchini kuanzia mtu binafsi, wafanyabiashara wadogo, wakati na wakubwa.
Hayo ameyasema Afisa Mwangalizi wa wateja wakubwa Benki ya EQUITY, Adams Marandu wakati akizingumza na waandishi wa Habari katika maonesho ya 47 ya Kimataifa ya biashara (Sabasaba) Jana Jijini Dar es salaam.
“Katika maonesho ya mwaka huu ujumbe wetu mkubwa ni TUMERAHISISHA, tumerahisisha biashara katika nyanja zote kwa wadau wote wa biashara nchini kuanzia mtu binafsi, wafanyabiashara wadogo, wakati na wakubwa”

Aidha Marandu amezitaja huduma zote za ndani ya Benki ya EQUITY ambazo zimerahisishwa ikiwemo ufunguaji wa akaunti, utaratibu wa kupata afisa mahususi, upatikanaji wa mikopo na kutoa elimu kuhakikisha kwamba huduma wanayoipata ni sahihi na yenye kutusaidia kukua.

Marandu amewakaribisha wananchi wote katika matawi ya Benki ya EQUITY nchini nzima ili wapate huduma na kupelekea kukuza uchumi wetu wa Tanzania.
More Stories
ZOLA yajipanga kupeleka Nishati Safi kwa Watanzania, yaunga Mkono Juhudi za Rais Samia
Kiongozi wa Mwenge awataka RUWASA kukamilisha mradi wa maji kwa wakati Kilindi
Balozi Nchimbi aongoza waombolezaji kumuaga Mzee Mongella