Na Mwandishi wetu, TimesMajira Online
Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa amelazimika kutoa viatu vyake vipya na kuwapa Mafundi na kumuagiza Mkandarasi anayeteleza ujenzi wa mradi wa barabara ya mzunguko wa nje ya Dodoma kuhakikisha ndani ya saa moja anatoa viatu vipya na vifaa vya usalama kwa mafundi mafundi wote katika mradi huo.

Bashungwa ametoa agizo hilo wakati akikagua utekelezaji wa ujenzi wa mradi wa barabara ya mzunguko wa nje ya Dodoma (Km 112.3) na kutoridhishwa na uchukuaji hatua za usalama kazini kwa wafanyakazi.
Aidha, Bashungwa amemuagiza Mtendaji Mkuu wa TANROADS, Eng. Mohamed Besta, kuhakikisha anasimamia usalama na afya za wafanyakazi mahali pa kazi katika maeneo yote yanapotekelezwa miradi ya ujenzi wa miundombinu kwa kutoa vifaa vya usalama ikiwemo kofia ngumu, viatu, gloves, reflector na barakoa za kuzuia vumbi.
More Stories
Kamishina TRA avitaka Viwanda viwili Mkuranga kulipa kodi inayostahili
Jimbo la Kibakwe wafanya ibada kuiombea nchi na viongozi wake
Naibu Meya Masaburi apewa uanachama wa heshima umoja wa LITONGO