March 7, 2026

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Mkurugenzi Tantrade atunukiwa Udaktari na London Institute of Skills Development and Oxford Club

Na Mwandishi wetu,Timesmajira

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade), Latifa Khamis ametunukiwa Shahada ya Heshima ya Udaktari wa Biashara na Uchumi kutokana na mchango wake mkubwa katika kukuza biashara na diplomasia ya uchumi kati ya Tanzania na nchi nyingine.

Tuzo hiyo imetolewa na London Institute of Skills Development and Oxford Club kama uthibitisho wa juhudi, umahiri na mafanikio ya Dkt. Latifa katika kusimamia kwa ufanisi majukumu ya TanTrade, ambayo yamechochea maendeleo ya sekta ya biashara nchini na kuimarisha ushirikiano wa kimataifa wa kiuchumi.