Na Zena Mohamed, Dodoma
BAADA ya malalamiko ya wafanyabiashara wengi jinsi ya kupata sehemu za kufanyia biashara katika maeneo ya stendi mpya ya mabasi, eneo la mapumziko Chinangali na Soko jipya, Halmashauri ya jiji la Dodoma imesema itaanza kutoa fomu za usajili kwa njia ya mtandao.
Hatua hiyo imekuja kufuatia Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma Godwin Kunambi kuanza kutoa maeneo hayo kwa njia ya kujaza fomu kwa njia ya mkono katika eneo la halmashauri ya zamani hali iliyosababisha msongamano wa watu wengi ambao walikuwa wakihitaji kujaza fomu hizo.
Hali hiyo ilimlazimu juzi Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Patrobas Katambi kufika katika eneo hilo na kusitisha utoaji wa fomu hizo kutokana na mkusanyiko mkubwa ambao aliutaja kuwa unahatarisha maisha kutokana na ugonjwa wa Corona.
Kutokana na hali hiyo ilimlazimu Mkurugenzi wa halmashauri ya jiji la Dodoma Godwin Kunambi kutangaza kwamba nafasi za maeneo ya kufanyia biashara zitaanza kutolewa kwa njia ya mtandao.
More Stories
Madaktari 1,109 kunufaika na ufadhili wa Rais Samia katika masomo ya ubingwa bobezi 2023/24
Kimbunga “HIDAYA”chazidi kuimarika
DC aeleza umuhimu wa mafunzo ya JKT