Na Mwandishi wetu, TimesMajira Online
KATIBU Mkuu wa Wizara ya Madini Nchini, Kheri Mahimbali, amesema Tanzania kwa sasa imeweka mazingira mazuri kwa wawekezaji kuja kuwekeza kwenye sekta ya madini kwa namna itakayofaidisha pande zote.
Mahimbali ameyasema hayo wiki hii wakati wa mkutano wa wadau wa sekta ya madini uliondaliwa na taasisi ya Chatham House na uliofanyika jijini London.

Katika mkutano huo, Katibu Mkuu Mahimbali amezungumzia umuhimu wa kuongezeka kwa uwekezaji kwenye madini ya kimkakati ambayo yako kwa wingi ambao uwekezaji wake umekuwa mdogo ukilinganisha na mahitaji yaliyopo hasa barani Afrika.
More Stories
RUWASA yakamilisha ujenzi wa visima Korogwe
Mch.Hananja awataka viongozi wa dini kuacha kutumia majukwaa ya kidini kwa kujitafutia umaarufu
Matiko atangaza nia ya kugombea Ubunge Kivule