Na Mwandishi wetu, TimesMajira Online
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, ameiagiza serikali yake kuhakikisha Serikali ya Mkoa na Kitengo cha Maafa cha Ofisi ya Waziri Mkuu kuweka makazi ya muda ya watu ambao makazi yao yamesombwa na maji kwa lengo la kuwastiri wananchi hao wilayani Hanang, mkoani Manyara, haswa katika vijiji vya Katesh, Jorodom, Ganana, Dumbeta, Gendabi, Sarijandu, Arukushay na Sebasi.
Kwa taarifa za awali nyumba na mifugo imeathirika sana huku idadi za kaya zilizoathirika ni 1,150, idadi ya watu walioathirika hadi sasa ni 5,600 na pia ikikadiriwa takriban ekari 750 za mashamba zimeharibika.




More Stories
Vyombo vya ulinzi na usalama Mbeya,Benki kuu kushirikiana kutatua changamoto za utapeli mtandaoni
Polisi Mbeya kuimarisha ulinzi kuelekea sikukuu ya Pasaka
BAKWATA yawazawadia washindi wakuhifadhi Qur’an