Na Mwandishi wetu, TimesMajira Online
Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan na Rais wa Zambia, Hakainde Hichilema wameazimia kuweka mazingira yatakayofanya biashara kati ya Tanzania na Zambia zisiwe na vikwazo.
Wakizungumza katika Kongamano la Wafanyabiashara wa Tanzania na Zambia lililofanyika jana jioni marais hao walisema eneo moja la muhimu ni kuhakikisha magari hayakai kwenye mipaka kwa muda mrefu pasi na sababu.
Marais hao wanakutana kwenye mkutano wa ana kwa ana leo asubuhi na waliwaambia Wafanyabiashara hao kwamba mazungumzo yao yatajikita kwenye kuweka taratibu za kuondoa changamoto hizo.





More Stories
Mch.Hananja awataka viongozi wa dini kuacha kutumia majukwaa ya kidini kwa kujitafutia umaarufu
Matiko atangaza nia ya kugombea Ubunge Kivule
TPTC kuendesha kozi ya Walinda Amani wa Kirai