Na Mwandishi wetu, TimesMajira Oline
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa Sh.milioni 10 kwa ajili ya kuwawezesha Wanawake wa Vikundi mbalimbali vya vicoba wilayani Kondoa Mkoani Dodoma.
Akizungumza wakati akikabidhi fedha hizo Mbunge wa Viti maalumu Mkoa wa Dodoma Mhe. Mariamu Ditopile alisema Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan anatambua jitihada za wanawake nchini katika kazi wanazozifanya kuhakikisha wanajikwamua kiuchumi.

“Rais Dkt. Samia anawapenda sana wana Kondoa na wakati nakuja hapa niliwasiliana nae akanikabidhi Sh.Milioni 10 na amesema fedha hizo zikabidhiwe kwa vikundi vya vicoba zikawasaidie wanawake kujiimarisha kiuchumi”
Katika hatua nyingine Ditopile aliahidi kuunga mkono jitihada za Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan za kumkomboa mwanamke kiuchumi kwa kuwachangia Sh.Milioni Tano.




More Stories
Lushoto watakiwa kumuunga mkono Rais Samia kuimarisha elimu
Zaidi ya bilioni 100 zatolewa kwa ajili ya madaraja 13,Lindi
Serikali kupeleka milioni 100 kwa ajili ya kituo cha afya Saranga