Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mary Masanja amewataka askari wa uhifadhi nchini kufanya kazi kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu ili kutekeleza majukumu yao ipasavyo kwa manufaa ya Taifa.
Ameyasema hayo jana katika kikao chake na Askari Uhifadhi alipotembelea Hifadhi ya Pori la Akiba Kijereshi lililoko wilayani Busega mkoani Simiyu.
Pia Masanja amewataka askari hao kushirikiana na wananchi katika kukabiliana na tatizo la tembo.
Kikao hicho kilihudhuriwa na Maafisa na Askari Uhifadhi kutoka Pori la Akiba Kijereshi na Kikosi dhidi ya Ujangili kutoka Bunda na Mkoa wa Mwanza.
Baadhi ya Maafisa na Askari Uhifadhi kutoka Pori la Akiba Kijereshi na Kikosi dhidi ya Ujangili kutoka Bunda na Mkoa wa Mwanza wakimsikiliza Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mary Masanja (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao alipotembelea Hifadhi ya Pori la Akiba Kijereshi lililoko Wilayani Busega mkoani Simiyu.Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mary Masanja akizungumza na Maafisa na Askari Uhifadhi alipotembelea Hifadhi ya Pori la Akiba Kijereshi lililoko Wilayani Busega mkoani Simiyu. Kushoto ni Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) Kanda ya Ziwa Laurent Katakweba na Meneja wa Pori la Akiba Kijereshi, Lusato Masinde (kulia)
More Stories
Lushoto watakiwa kumuunga mkono Rais Samia kuimarisha elimu
Zaidi ya bilioni 100 zatolewa kwa ajili ya madaraja 13,Lindi
Serikali kupeleka milioni 100 kwa ajili ya kituo cha afya Saranga