Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Amos Makalla amemuelekeza Afisa Elimu wa Mkoa huo kuhakikisha kuanzia Sasa Vijana wa Scout wanashirikishwa Katika shughuli mbalimbali na sio kusubiri yatokee Matukio ya Majanga, Mikutano, ugeni wa Viongozi au Misiba ndipo umuhimu wao unaonekana.
RC Makalla ametoa maelekezo hayo wakati alipotembelewa ofisini kwake na Kamishina wa Scout Dar es salaam alieambatana na Watendaji wa TAKUKURU na kukabidhiwa Kitabu Cha Mwongozo wa mafunzo kwa wawezeshaji kufundisha Vijana wa Scout kuhusu kuzuia na kupambana na Rushwa.

More Stories
Kanisa la Shincheonji la Yesu nchini Ufaransa lakanusha ripoti ya Le Parisie
Vyombo vya ulinzi na usalama Mbeya,Benki kuu kushirikiana kutatua changamoto za utapeli mtandaoni
Polisi Mbeya kuimarisha ulinzi kuelekea sikukuu ya Pasaka