Na Abdulrahman Salim,TimesMajira Online. Rukwa
OFISI ya Ardhi Mkoa wa Rukwa, inaendelea na zoezi la kufanya uhakiki wa maeneo ya wazi na ya umma yaliyoorodheshwa kwa mujibu wa ramani za mipango miji za halmashauri za mkoa huo, ili kubaini endapo kuna uvamizi umefanyika katika maeneo hayo.
Akizungumza kuhusiana na zoezi hilo Kamishna Msaidizi wa Ardhi Mkoa wa Rukwa, Swagile Msananga amesema lengo la kufanya zoezi hilo ni kupata orodha kamili ya meneo ya wazi, ili yaweze kutambulika rasmi huku akiwaonya wananchi waliovamia katika maeneo hayo.
“Kwa maeneo ambayo yatakuwa yamevamiwa, kutakuwa hakuna namna ya kufanya isipokuwa wavamizi wataondolewa, ili kupisha maeneo ya wazi kwa sababu yanatakiwa yalindwe kwa nguvu zote na maeneo ambayo yapo salama mpaka sasa hivi, tutahakikisha mipaka yake inawekwa bayana na wananchi watatakiwa waiheshimu,” amesema.
Ameongeza kuwa baada ya kupata orodha kamili ya maeneo hayo atakabidhiwa Mkurugenzi, ili aweze kuyaandalia hati kwa ajili ya ulinzi wa maeneo hayo kwa siku za usoni.

More Stories
Senyamule:Serikali inapaswa kuzitambua Kampuni zinazofanya biashara ya ardhi
Serikali kuendelea kupanua fursa elimu Singida
Kumekucha CDF Cup 2026, NMB yaweka Sh milioni 150