RAIS John Pombe Magufuli leo ameapishwa kuwa rais wa Tanzania kwa awamu ya pili baada ya kutetea nafasi yake na kushinda kwa kishindo katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba 28,mwaka huu.
Rais Magufuli alishinda kwa kupata kura 12,516,252 ambayo ni asilimia 84 ya kura zote zilizopigwa. Tundu Lissu kutoka chama cha upinzani cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ameshika nafasi ya pili kwa kupata kura 1,933,271 ya kura zote zilizopigwa.
Rais Magufuli ni rais wa tano kuiongoza Tanzania kuanzia mwaka 2015 mpaka 2020 na sasa anatarajia kuongoza mpaka mwaka 2025.
More Stories
Mramba akagua jengo la Wizara ya Nishati Mtumba
Serikali yathamini mchango wa viongozi wa Dini kwenye maendeleo
Waziri Jafo awaasa wajumbe Bodi ya FCC kuwa waadilifu, waaminifu