Na Mwandishi wetu.Timesmajira
Airtel Africa imepata faida baada ya kodi ya Dola za Marekani 586 milioni kwa kipindi cha miezi tisa kilichoisha Desemba 31, 2025, ikiongezeka zaidi ya mara mbili kutoka Dola 248 milioni katika kipindi kilichotangulia, ikichangiwa na faida kubwa za uendeshaji na mapato makubwa kifedha na mabadiliko ya fedha za kigeni.
Katika kipindi hicho, faida ya uendeshaji na mabadiliko ya fedha za kigeni yenye thamani ya Dola 99 milioni ikilinganishwa na hasara ya Dola 153 milioni katika kipindi kilichotangulia, ilichangiwa sana na utendaji wa kifedha wa Airtel Africa.
Ndani ya kipindi cha miezi tisa mapato yalifikia Dola 4,667 milioni, yakiongezeka kwa asilimia 24.6 kwa thamani ya sarafu thabiti na asilimia 28.3 kwa thamani iliyoripotiwa kutokana na kuimarika kwa sarafu, jambo lililoimarisha misingi ya biashara.
Utekelezaji makini wa mkakati wa Airtel Africa ulipelekea ongezeko la mapato hadi asilimia 24.7 katika Robo ya 3, 2026, jambo lililosaidiwa zaidi na kuimarika kwa sarafu, ambapo ongezeko la mapato liliripotiwa kuwa asilimia 32.9.
Katika muhula huo mapato ya huduma za simu yaliongezeka kwa asilimia 23.3 kwa sarafu thabiti. Mapato ya data, ambayo ndiyo yanayochangia zaidi kwenye mapato ya kundi, yaliongezeka kwa asilimia 36.5 huku mapato ya sauti yakiongezeka kwa asilimia 13.5.
Mapato ya Mobile Money yanaendelea kukua, yakipeleka ongezeko la asilimia 3.4 kwa sarafu thabiti. Airtel Money imeendelea kuonyesha ukuaji imara katika mhura huu, ikiipita mafanikio mawaili muhimu.
Idadi ya wateja iliongezeka kwa asilimia 17.3 hadi milioni 52.0, huku thamani ya jumla ya malipo yaliyosindikwa kwa mwaka (TPV) kwa Robo ya 3, 2026 ikipita Dola bilioni 210.
Mfumo mpana zaidi na ukuaji wa matumizi ya kidijitali pia ulisababisha ongezeko la asilimia9.8 kwenye ARPU kwa sarafu thabiti.Kutambua fursa kubwa katika masoko yake, Airtel Africa iliweka mkazo wa uwekezaji kulingana na miongozo ya capex iliyorekebishwa iliyotangazwa awali.
Matumizi ya mtaji yalifikia Dola 603 milioni, yakiongezeka kwa asilimia 32.2 kutoka kipindi kilichotangulia, na kusaidia upanuzi wa takriban minara 2,500 mipya na upanuzi wa mtandao wa nyuzi za kioo kwa takriban km 4,000, hivyo kufikia jumla ya km 81,500.
Uwekezaji huu umeimarisha upanuaji na uwezo wa mtandao, ukisaidia kuboresha uzoefu wa wateja.
Jumla ya ufikiaji wa idadi ya watu ulifikia asilimia 81.7, ongezeko la alama asilimia 0.6kutoka mwaka uliopita.
Akizungumza kuhusu matokeo hayo, Mkurugenzi Mtendaji wa Airtel Africa, Sunil Taldar, alisema:“Matokeo haya yanaonyesha nguvu ya mkakati wetu, yakionyesha utendaji thabiti wa uendeshaji na kifedha katika biashara zetu zote.”
Katika robo hii, kampuni ilikazia uwekezaji ili kuongeza upanuzi wa mtandao na uwezo wa data huku ikipanua mtandao wake wa nyuzi za kioo. Uwekezaji huu, ukiunganishwa na ushirikiano wa ubunifu, unaleta nguvu zaidi kwa wateja na unatuweka katika nafasi ya kunasa fursa kubwa za ukuaji katika masoko yetu.
Ameongeza kuwa kidijitali, ubunifu wa kiteknolojia, na kuingizwa kwa AI katika uendeshaji vitaimarisha uzoefu wa wateja, kupanua huduma za kidijitali, na kuunganisha vyema huduma za GSM na Airtel Money, hivyo kuwezesha kampuni kukidhi mahitaji yanayoongezeka.
Uchukuzi wa simu mahiri unaendelea kuongezeka, ukiwa na kiwango cha penetration ya asilimia 48.1 huku biashara ya home broadband ikionyesha ukuaji imara, ikionyesha mahitaji yanayoongezeka ya muunganisho wa kasi ya juu na wa kuaminika.
“Juhudi zetu za kuongeza ujumuishaji wa kifedha barani Afrika zinaendelea kupata mwendo mzuri, huku idadi ya wateja wa Mobile Money ikifikia milioni 52, ikipita milestone ya milioni 50,” amesema.
Thamani ya jumla ya malipo yaliyochakatwa (TPV) ya Dola bilioni 210 kwa Robo ya 3, 2026 inaonyesha ukubwa na kina cha wajasiriamali, mawakala, na washirika, ikithibitisha nafasi ya Airtel kama kielelezo muhimu cha ujumuishaji wa kifedha barani Afrika.
Kampuni ipo kwenye mstari sahihi kwa ajili kuiorodhesha Airtel Money katika nusu ya kwanza ya 2026.
“Mkakati wetu wa kuzingatia wateja unaendesha mwendo mzuri, ukiungwa mkono na uwekezaji wa mtandao, kidijitali, na ushirikiano wa kimkakati,” ameongeza.
Idadi ya wateja jumla iliongezeka kwa asilimia 10 hadi milioni 179.4, huku watumiaji wa data wakiongezeka asilimia 14.6 hadi milioni 81.8.

More Stories
Usajili wa Laini za Simu: Jilinde Dhidi ya Kutumiwa Vibaya kwa Utambulisho Wako
TTCL yaadhimisha siku ya Wanawake kwa kutoa msaada JKCI
Wananchi Dodoma washauri TBA kujenga nyumba za kupangisha watu binafsi