March 7, 2026

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Mwanasheria Mkuu wa Serikali Johari awasilisha Azimio la Bunge la kumthibitisha Waziri Mkuu

Na Mwandishi wetu,Timesmajira

Mwanasheria Mkuu wa Serikali Hamza Johari akiwasilisha Azimio la Bunge la kumthibitisha Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Bungeni Jijini Dodoma, tarehe 13 Novemba, 2025.

Mwanasheria Mkuu wa Serikali amewasilisha Azimio hilo mbele ya Bunge kufuatia uteuzi uliofanywa na Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa kumteua,Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.