Na Mwandishi wetu, TimesMajira Online
MSANII wa uigizaji katika tasnia ya filamu nchini, Chuchu Hansi, amesema kuwa ni jambo la busura kuwambuka wasanii ambao wametangulia mbele ya haki na kuendeleza mazuri yao.
Chuchu amesema hayo muda huu, katika shughuli ya kuwakumbuka wasanii mbalimbali wakiwemo watangazaji na watozi wa filamu waliofariki dunia ambayo umefanyika jijini Dar es Salaam.
Pia amefafanua kuwa katika kuenzia mazuri ya wasanii waliofariki dunia, ameshirikisha baadhi ya wasanii waliokwenye kituo cha Sanaa cha Mzee Majuto kilichoko jijini Tanga.
“Ndio wapo baadhi ya wasanii ambao nimewashirikisha kutoka kwenye kituo cha Mzee Majuto na ‘soon’ mtaweza kuwaona pindi itakapoanza kuoneshwa katika kituo cha runinga nilipoipeleka, amesema.

More Stories
TAMWA yakumbusha jamii kupinga ukatili wa kijinsia kuelekea siku ta wanawake Duniani
Wanawake washauriwa kuchangamkia fursa za uchumi
Aida:Wanawake wakipata haki zote itapunguza migogoro